Tenor inajumuisha programu ya vifaa vya mkononi ya Tenor, tovuti ya Tenor inayopatikana katika http://tenor.com, viendelezi vya Tenor na API ya Tenor. API ya Tenor inaweza kuunganishwa na vifaa au huduma nyingine, lakini huduma zozote zinazohusiana na Tenor zinatolewa na Google.
Ili utumie Tenor, ni sharti ukubali (1) Sheria na Masharti ya Google na (2) Sheria na Masharti haya ya Ziada ya Tenor ("Masharti ya Ziada ya Tenor").
Tafadhali soma kwa makini hati hizi zote. Kwa pamoja, hati hizi zinajulikana kama "Masharti". Zinaelezea kile unachoweza kutarajia kutoka kwetu pale unapotumia huduma zetu na kile tunachotarajia kutoka kwako.
Iwapo Masharti haya ya Ziada ya Tenor yanakinzana na Sheria na Masharti ya Google, Masharti haya ya Ziada yatatumika kusimamia Tenor.
Ingawa si sehemu ya Masharti haya, tunakuhimiza usome Sera yetu ya Faragha ili uelewe zaidi jinsi unavyoweza kusasisha, kudhibiti, kuhamisha na kufuta maelezo yako.
1.
Maudhui yako.
Tenor inakuwezesha kuwasilisha, kuhifadhi, kutuma, kupokea au kushiriki maudhui yako. Google ina leseni ya kutumia maudhui yako kama ilivyofafanuliwa kwenye Sheria na Masharti ya Google, hivyo endapo utapakia maudhui kwenye Tenor, tunaweza kuonyesha maudhui hayo kwa watumiaji na kuyashiriki pale tutakapoelekezwa, na watumiaji hao (ikijumuisha watumiaji wanaofikia maudhui kupitia API ya Tenor) wanaweza kutazama, kushiriki na kurekebisha maudhui hayo.
2.
Maudhui yaliyopigwa marufuku.
2.1
Usitumie Tenor kwa dhumuni lolote la kibiashara au kwa manufaa ya wengine.
2.2
Kama tulivyofafanua kwenye Sheria na Masharti ya Google, tungependa kudumisha mazingira yenye heshima kwa kila mtu. Unapotumia Tenor, ni lazima ufuate Sera Zetu za Mpango na kanuni za msingi za matendo zilizofafanuliwa kwenye Sheria na Masharti ya Google. Hususani, pale unapotumia Tenor, hutakiwi:
i. yanakiuka au yanashawishi mwenendo wowote ambao utakiuka sheria zinazotumika au haki za wengine, ikijumuisha maudhui yoyote ambayo yanakiuka, yanatumia vibaya au yanakiuka haki za uvumbuzi za mtu mwingine au haki za utangazaji au faragha;
ii. yanajumuisha maelezo binafsi au anwani ya mawasiliano kuhusu watu wengine bila uidhinishaji wao;
iii. yanahimiza shughuli hatarishi au zisizo halali au vitu vilivyozuiliwa;
iv. yana ulaghai, udanganyifu au upotoshaji;
v. ni uongo au yanakashifu;
vi. ni machafu au ya kiponografia;
vii. yanahamasisha au yanajumuisha ubaguzi, ushabiki, ubaguzi wa rangi, chuki, unyanyasaji au madhara kwa mtu binafsi au kikundi;
viii. ni ya vurugu au yanatishia au yanahamasisha vurugu au vitendo vinavyotishia mtu binafsi, kikundi au shirika; au